Watani
wa jadi wameshindwa kutambiana baada ya kutoka kwa sare ya 1-1 katika
pambano la kusisimua uwanja wa Taifa. Simba walikuwa wa kwanza
kuzifumania nyavu kwa bao la Amri Kiemba alieunganisha kazi nzuri ya
Mwinyi Kazimoto wakati Yanga walisawazisha kipindi cha pili kwa mkwaju
wa Penati uliofungwa kifundi na Said Bahanuzi baada ya beki Paul Ngalema
kuunawa mpira kwenye eneo la hatari. Yanga walilazimika kucheza robo ya
mwisho wakiwa pungufu baada ya Simon Msuva kupewa kadi nyekundu kwa
kumchezea ndivyo sivyo Juma Nyoso. Hadi kipenga cha mwisho kinapulizwa
Yanga 1-1 Simba.
No comments:
Post a Comment