Kwanza kabisa ni vema ikaeleweka kwamba mradi ambao wawekezaji kutoka China na Oman walikuwa tayari kuutekeleza unajulikana kama Bagamoyo Special Economic Zone- kwa kiswahili - Eneo la Ukanda Maalum wa Uchumi Bagamoyo. Ujenzi wa Bandari- ni moja ya component Nne za Mradi huo mkubwa. Component nyingine za mradi ni ujenzi wa eneo la viwanda (industrial park) ambalo katika awamu ya kwanza litakuwa na viwanda 190 vitakavyozalisha ajira mpya za moja kwa moja 20,000 na awamu ya pili na tatu ikikamilika kutakuwa na viwanda 790- zitakazozalisha ajira mpya 100,000.
Component ya tatu ni ujenzi wa mji wa kasisasa wa makazi unaonendana na mahitaji ya karne ya 21. Ujenzi wa mji huu utasaidia kupunguza msongamano wa jiji la Dar es saalaam kwani shughuli nyingi za uchumi zitakazotokana na Bagamoyo Speciam Economic Zone zitapelekea watu wengi kuhamia kutoka Dar es salaam kwenye mji mpya.
Component ya nne ni logistics Park ambayo itafanya bagamoyo kuwa kitovu cha usaifirishaji wa mizigo na hivyo kuimarisha Tanzania kama transit route ya mizigo inayotoka na kuingia kwenda sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi- hii logistic park ndio ita handle transshipment kutoka Afrika kwenda Ulaya na Marekani
Concept ya mradi huo imefanana na concept ya mradi wa Shenzen- Special Economic Zone ambayo Kampuni inayotaka kuwekeza Bagamoyo ilikuwa mojawapo ya kampuni zilizowekeza
Bahati mbaya watu wengi wanajikita kuzungumzia bandari na huenda hata maamuzi ya kuukata mradi yamefanyika kwa kuzingatia component moja tu ya bandari na wameacha kufikiria manufaa makubwa ya ajira hasa kipindi hiki ambacho vijana wengi wa Tanzania wanamaliza shule bila matumaini ya kuajiriwa.
Mradi huo mkubwa umekuwa gumzo sehemu mbalimbali ulimwenguni kutokana na ukubwa wake pamoja na athari zake kwa maslahi ya makundi mbalimbali ulimwenguni.
Kwa mataifa ya Magharibi mradi huo ulikuwa tishio kwa consideration za ushindani na ushawishi ndani ya ukanda wa bahari ya Hindi ambao unabashiriwa kuwa kitovu muhimu katika bishara ya kimataifa katika miaka michache ijayo. Wazungu waliuona mradi huo utaipa China nguvu kubwa zaidi ya kiuchumi.
Kwa mataifa mengine kama Afrika ya Kusini - mradi huo ulikuwa tishio kwa maslahi yao ya kiuchumi kwakuwa ungepelekea ushindani mkubwa kwa Biashara ya Bandari ya Durban ambao hivi sasa ndio kuna bandari pekee zenye uwezo wa kuhandle 4th generation ships.
Kwa Kenya, mradi wa Bagamoyo ulikuwa ni tishio kubwa kwa mradi wa Bandari mpya wanayopanga kuijenga huko LAMU ambayo itakuwa na uwezo wa kuhandle 4th generation ships na pia itakuwa na kitovu cha usafirishaji wa mafuta barani Afrika
Benki ya Dunia - nayo imekuwa negative juu ya mradi huo - na imetumia influence yake kwa Serikali kutokana na misaada na mikopo ambayo inaipatia Tanzania, kupenyeza ushawishi wa kuupinga mradi. Inafahamika Benki ya Dunia ni chombo kinachotumika na mataifa ya magharibi kutingisha serikali za Afrika pale zinapokiuka interest za wakubwa. Tumeona jinsi walivyoibana serikali kutizama
Upya baaadhi ya sheria zake mpya ili iweze kutoa ahadi za mikopo. Hoja waliyotoka nayo kupinga mradi wa Bagamoyo ni kwamba - kwakuwa wao wameipa Serikali mkopo wa maboresho ya bandari ya Dar es salaaam- endapo mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone utatekelezwa, utaleta ushindani kwa Bandari ya Dar es salaam na hivyo kushindwa kulipa mkopo.
Makundi haya matatu yalikuwa na common interest ya kuhakikisha kwamba Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone hautekelezwi. Imetumika nguvu kubwa ya ushawishi kwa kutumia propaganda za vyombo vya habari; economic intelligence; political influence & scare mongering techniques kuhakikisha mradi huu hausimami. Kazi waliyoifanya kwa mafanikio makubwa.
Ni vizuri kuzichambua hoja zinazotolewa dhidi ya mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone ili kuona kama kuna mantiki.
Hofu ya Serikali kupoteza mapato kutokana na ushindani wa Bandari ya Bagamoyo
Ukiangalia kwa juu juu hoja hiyo ina mantiki. Kwamba kutakuwa na ushindani na Dar es salaam itapoteza mapato. Lakini yapo mambo matatu yanayothibitisha kwamba hoja hiyo sio sahihi.
1) Bandari ya Bagamoyo itahudumua meli kubwa (4th generation ships) ambazo hivi sasa haziwezi kuingia katika bandari ya Dar es salaam. Katika biashara ya kimataifa hivi sasa, usafirishaji kwa kutumia meli kubwa ndio wenye tija, unafuu na faida. Kwa mfano leo hii kusafirisha bidhaa X kutoka Tanzania hadi China au Marekani kwa kutumia meli ndogo inagharimu mara mbili ya gharama ya usafirishaji kwa meli kubwa. Kutokuwa na uwezo wa ku handle meli kubwa kumefanya gharama za usafirishaji wa bidhaa kutoka Nchi zetu kwenda kwenye masoko kuwa kubwa (uncompetitive). Ndio maana leo hii nchi za Latin America ambazo zipo mbali kabisa na China, zinauza bidhaa zake nyingi katika soko la China kuliko nchi za Afrika ambazo zipo karibu na China kijiografia. Mfano halisi umetokea majuzi- Marekani ilipoanza vita ya biashara na China kwa kuongeza kodi katika bidhaa za China, in response China waliongeza kodi kwa maharage ya soya kutoka Marekani. Ikumbukwe kwamba biashara ya soya ni kubwa sana kwa Marekani- kila mwaka wanauza soya ya thamani ya Usd 35 Billion na zaidi kwa China. Hivyo kitendo cha China kuongeza kodi, gharama za soya zikapanda na hivyo wanunuzi wa soya kutoka China walitafuta altenative source ya soya- badala ya kuja Afrika, walikwenda Latin Amerika- moja ya sababu ya kwenda kule pamoja na mambo mengine ni uwepo wa bandari zenye uwezo wa kuhandle meli kubwa ambazo ni nafuu katika usafirishaji. Afrika imekosa fursa ya biashara kubwa sababu hiyo.
2) Uwepo wa bandari kubwa katika eneo moja huongeza wingi wa shughuli za usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye bandari kubwa kwenda kwenye bandari ndogo. Mzigo mkubwa ambao ungeshushwa Bagamoyo ungetengeneza fursa ya biashara kwa meli ndogo na za kati kuuchukua Bagamoyo na kuupeleka kwenye bandari za jirani za Dar, Tanga, Mombassa, Beira nk
3) Ni vizuri pia kujiuliza hicho tunachoki protect (Katika Bandari ya Dar) manufaa yake ni zaidi ya manufaa tutakayopata katika Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone? Hivi sasa hivi Bandari ya Dar es salaam inaajiri watu wangapi? Baada ya upanuzi utakaofanywa ajira ngapi zitaongezeka? Ukweli ni kwamba kwa teknolojia za karne ya 21 shughuli za bandari zipo digitalized sana kiasi kwamba ile asili ya kuzalisha ajira nyingi haipo tena. Hivyo kwa vyovyote vile ajira mpya zitakazozalishwa baada ya kumalizika upanuzi hazitozidi 1000. Kwa upande mwingine, ajira zitakazozalishwa kwenye mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone- katika awamu ya kwanza tu ni 20,000. Je faida ipi wapi?
Kwa upande wa mapato (direct income) kwa Bandari ya Dar es salaam- serikali inapata kiasi gani? Kwa vyovyote vile mapato ya jumla ambayo serikali itakayapata katika mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone yatakuwa ni makubwa zaidi- kwani mbali na mapato itakayopata katika component ya bandari kwa njia ya Whaphage charges; import duties kwa bidhaa nyingi zitakazopitia katika bandari hiyo- serikali itapata kodi za aina mbalimbali katika viwanda 190 na baadyad 790 vitakavyojengwa. Watumishi 20,000 tu pay as you earn yao itakuwa ni kiasi kikubwa cha uhakika kwa serikali. Achilia mbali multiplier effects zitokanazo na shughuli za viwanda. Katika mji mpya utakaojengwa Serikali itapata kodi za majengo na kodi nyingine zitokanazo na ardhi na pango... achilia mbali kodi za shughuli nyingine za biashara zitakazofanyika Bagamoyo.
Hoja nyingine inayotolewa ni kwamba kumpa mgeni aendeshe bandari ni hatari kwa usalama wa nchi. Hapa cha kujiuliza- ndani ya Bandari ya Dar es salaam kuna kampuni ya Nje TICTS imeendesha shughuli zake ndani ya bandari kwa miaka 20 na zaidi - ni usalama upi umeathirika?
Inapokuja kwa hoja za kiusalama, China inamahusiano ya karibu sana ya kijeshi na Tanzania. Kila leo tumeona vikifunguliwa vyuo, viwanja vya ndege nk kwa msaada wa China. Wanajeshi wengi wa Tanzania wamepata mafunzo China na vifaa vingi vya kivita vimetoka China. Ni jambo la kawaida kukuta gari yenye number za JWTz ndani yake kuna askari wa Tanzania na China... sasa kwa ukaribu huo wa kihistoria tangu JWTZ ilipoanzishwa baada ya kuvunja jeshi lenye asili ya kikoloni lililojaribu kufanya mapinduzi miaka ya 60, leo hii sisi ndio watu wa kuhofia usalama dhidi ya Wachina?
Hoja nyingine inayozungushwa ni kwamba eti Wachina watanya'ngyanya mali za taifa endapo mradi huo utapata hasara kama ilivyokuwa kwa mradi wa Bandari wa Sri Lanka. Ukweli ni kwamba mradi wa Bagamoyo sio sawa na mradi wa Sri Lanka au mradi wa ujenzi wa Reli ya Kenya. Tofauti na miradi hiyo miwili ya Kenya na Sri Lanka, mradi wa Bagamoyo unatekelezwa kwa njia ya uwekezaji kwa asilimia 100- wakati ile miradi ya Kenya na Sri Lanka inatekelezwa kwa mikopo ambayo nchi inawajibu wa kuweka dhamana (sovereign guarantee). Maana yake nini? Hata kama mradi wa Bagamoyo utapata hasara, atakayeumia ni mwekezaji na sio Serikali. Lakini kwa uzoefu wa kampuni ya China Merchant katika uwekezaji wa miradi mikubwa ya aina hii, haiwezekani wakafanya uamuzi wa kuwekeza mradi wa kupata hasara kirahisi namna hiyo. Ikumbukwe kwamba kampuni ya China Merchant ina uwezo wake kimtaji unaofikia mara 20 ya GDP ya Tanzania.
Hoja nyingine inayosemwa eti masharti ya kuendesha mradi wa bagamoyo ni magumu. Hivi mahala ambapo watu wanazungumza- kila upande una wajibu wa kuja na mapendekezo yake (proposal) na upande wa pili una haki ya kuja na counterproposal. Kuweka mpira kwapani sio njia sahihi. Kama serikali iliweza kwenda extra mile kuvutia mradi wa Bomba la Mafuta la Uganda kwa kutoa vivutio maalum vilivyopelekea hadi kufanyika mabadiliko ya sheria Bungeni- under miscleneous ammendment? iweje ishindwe kufanya hivyo kwa Mradi wa Bagamoyo? Kwa faida za ajira na kodi zinazokuja na mradi wa Bagamoyo kwa hakika zinazidi faida za mradi wa bomba la mafuta ambalo sehemu kubwa ya ajira zake zitatokea wakati wa ujenzi wa bomba lenyewe na likishakamilika ajira zitapungua kwa asilimia 80.
Ukiachilia faida za moja kwa moja zilizotajwa kuhusu mradi wa Bagamoyo, ni wazi kwamba ujenzi wa mradi huo pia utasaidia kuufanya mradi wa reli ya Kati ya Standard Gauge kupata idadi kubwa ya mizigo ya kusafirisha ili uweze kurejesha mikopo iliyochukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo.
Kwa ujumla na vyovyote iwavyo, faida za mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone ni kubwa kuliko madhara tunayodhani tunayaepuka
Search This Blog
Monday, May 13, 2019
Friday, April 26, 2019
RIPOTI YA CAG KUHUSU SARE ZA JESHI, UKURASA No 310
Ripoti ya CAG kuhusu sare za Jeshi ,Kurasa No. 310
Moja ya maelezo ya CAG.
" Kukosekana kwa nyaraka za kuthibitisha uletaji wa mzigo. Niliomba Hati ya kupokelea Shehena ya Mzigo Bandarini (Bill of Lading), Hati ya Madai kutoka kwa Mtengenezaji (Commercial Invoice), Hati ya Mzigo ulipotoka (Certificate of Origin), orodha za mali zilizopo kwenye meli (Packing List) na cheti cha ukaguzi wa bidhaa (Inspection Certificate) kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders kwa ajili ya kujiridhisha kama bidhaa husika zililetwa nchini. Hata hivyo, Mzabuni alishindwa kuwasilisha nyaraka hizo.
Aidha, nilipitia Mfumo wa Forodha (TANCIS)
wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na kubaini kuwa hapakuwa na shehena yoyote kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders mwezi Novemba 2015. d) Vilevile, nilifanya mahojiano na Maofisa wa Bohari kuu ya Jeshi la Polisi na kubaini hakukuwa na Sare zozote zilizoletwa na Mzabuni Daisy General Traders mwezi Novemba 2015. Hivyo, Serikali imepata hasara kubwa kwa kufanya malipo ya Sare za Polisi ambazo hazikuletwa na Mzabuni. Kuhusu suala hili, nashauri Mzabuni Daissy General Traders arejeshe kiasi alicholipwa kwa kutoleta Sare za Polisi na hatua stahiki za kinidhamu na kisheria zichukuliwe kwa Maofisa wote wa Jeshi la Polisi kwa kuisababishia Serikali hasara. "
Moja ya maelezo ya CAG.
" Kukosekana kwa nyaraka za kuthibitisha uletaji wa mzigo. Niliomba Hati ya kupokelea Shehena ya Mzigo Bandarini (Bill of Lading), Hati ya Madai kutoka kwa Mtengenezaji (Commercial Invoice), Hati ya Mzigo ulipotoka (Certificate of Origin), orodha za mali zilizopo kwenye meli (Packing List) na cheti cha ukaguzi wa bidhaa (Inspection Certificate) kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders kwa ajili ya kujiridhisha kama bidhaa husika zililetwa nchini. Hata hivyo, Mzabuni alishindwa kuwasilisha nyaraka hizo.
Aidha, nilipitia Mfumo wa Forodha (TANCIS)
wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na kubaini kuwa hapakuwa na shehena yoyote kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders mwezi Novemba 2015. d) Vilevile, nilifanya mahojiano na Maofisa wa Bohari kuu ya Jeshi la Polisi na kubaini hakukuwa na Sare zozote zilizoletwa na Mzabuni Daisy General Traders mwezi Novemba 2015. Hivyo, Serikali imepata hasara kubwa kwa kufanya malipo ya Sare za Polisi ambazo hazikuletwa na Mzabuni. Kuhusu suala hili, nashauri Mzabuni Daissy General Traders arejeshe kiasi alicholipwa kwa kutoleta Sare za Polisi na hatua stahiki za kinidhamu na kisheria zichukuliwe kwa Maofisa wote wa Jeshi la Polisi kwa kuisababishia Serikali hasara. "
SIKU YA HASARA(DAY OF LOSS)
" DAY OF LOSS"
---SIKU YA HASARA---
1) Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikiuwawawa ( state death).
2. Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo wazanzibar walipoteza mamlaka ( sovereignty) ya nchi yao.
3).Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Wazanzibar walipoteza uraia ( citizenship) wao wa Zanzibar.
4). Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar alikoma ( cease) kuwa Amiri Jeshi Mkuu.
5) Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Wanzanzibar walipoteza kiti chao Umoja wa MATAIFA.
--ZANZIBAR IMETOKA KUWA DOLA HADI KUWA MKOA--
-- UZANZIBAR UMETOKA KATIKA HADHI YA URAIA HADI KUWA UKAAZI ( Raia wa Zanzibar hadi Mzanzibari mkaazi)
--Kutoka Amiri Jeshi Mkuu hadi Kamanda Mkuu wa Idara maalumu--
-- Kutoka Rais wa Dola ya Zanzibar hadi Waziri asiye na Wizara maalumu--
--ZANZIBAR kutoka mwanachama wa Umoja wa Mataifa kukataliwa kujiunga na FIFA
TAREHE 24/4/1964 ni SIKU YA HASARA (DAY OF LOSS) KWA WAZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA UTAIFA WAO WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOCHEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA DOLA YAO JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA URAIA WAO WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA UTAMBULISHO WA DOLA YAO
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KILICHOWEZA--KINACHOWEZA AU KITAKACHOWEZA KUFIDIA HASARA WALIYOIPATA WAZANZIBAR TAREHE 26/4/1964
SIKU YA MAOMBOLEZI
---SIKU YA HASARA---
1) Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikiuwawawa ( state death).
2. Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo wazanzibar walipoteza mamlaka ( sovereignty) ya nchi yao.
3).Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Wazanzibar walipoteza uraia ( citizenship) wao wa Zanzibar.
4). Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar alikoma ( cease) kuwa Amiri Jeshi Mkuu.
5) Tarehe 26/4/1964 ndio siku ambayo Wanzanzibar walipoteza kiti chao Umoja wa MATAIFA.
--ZANZIBAR IMETOKA KUWA DOLA HADI KUWA MKOA--
-- UZANZIBAR UMETOKA KATIKA HADHI YA URAIA HADI KUWA UKAAZI ( Raia wa Zanzibar hadi Mzanzibari mkaazi)
--Kutoka Amiri Jeshi Mkuu hadi Kamanda Mkuu wa Idara maalumu--
-- Kutoka Rais wa Dola ya Zanzibar hadi Waziri asiye na Wizara maalumu--
--ZANZIBAR kutoka mwanachama wa Umoja wa Mataifa kukataliwa kujiunga na FIFA
TAREHE 24/4/1964 ni SIKU YA HASARA (DAY OF LOSS) KWA WAZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA UTAIFA WAO WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOCHEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA DOLA YAO JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA URAIA WAO WA ZANZIBAR
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KINACHOWEZA KUFIDIA WAZANZIBAR KUPOTEZA UTAMBULISHO WA DOLA YAO
HAKUNA KITU CHOCHOTE DUNIANI KILICHOWEZA--KINACHOWEZA AU KITAKACHOWEZA KUFIDIA HASARA WALIYOIPATA WAZANZIBAR TAREHE 26/4/1964
SIKU YA MAOMBOLEZI
NCHI TAKATIFU (HOLLY LAND)
Nchi Takatifu ( Holly Land)
Kabla hujawa kama ulivyo tunaambiwa alikuwepo Mungu tu au kwa jina unaloweza kumwita kwa mazoea yako. Mungu ndiye Baba wa wote, aliye juu ya yote, aliye katika yote, na ndani ya yote. Bila yeye hakuna kinachokuwa kama kilivyo. Imeandikwa alifinyanga udongo na kupuliza ndani yake roho wa uhai, kisha binadamu akawa nafsi hai. Mungu aliye roho anaingia katika nyumba aliyoifinyanga mwenyewe. Tukiondoa roho wa Mungu aletaye uhai ndani yako wewe ni nchi, wewe ni udongo. Kwa Mungu aliye mtakatifu sana kuamua kuacha utukufu wake na kujihengea nyumba ya udongo na kisha kukaa huko, wewe umefanyika nchi Takatifu ( Holly Land), give thanks to God. Mpe utukufu Mungu wewe ni wa kipekee you are gods na kati yenu hakuna aliye zaidi ya mwingine.
Acha kuheshimu au kuhangaika kutafuta nchi takatifu, wewe ndiye nchi takatifu. Acha kutafuta mahala patakatifu pa kuhiji wewe ndiye mahala penyewe alipopachagua Mungu.. hiji ndani yako na endelea kumtolea Mungu Dhabihu za shukrani. Utu wako ndiyo maskani yake Mungu ambayo yanapendeza kama nini? Je unayatamani makao ya Bwana? Ingia rohoni mwako kutana Naye maana imeandikwa je hamjui kwamba ninyi ni hekalu la roho mtakatifu. Mungu ni roho na ajili yake wewe upo na kwa njia yake ukafanyika kuwa kama ulivyo. Wewe ni maskani matakatifu ya Mungu mwenyewe. Acha kukimbiakimbia kumtafuta kule na kule, yeye yupo ndani ya nyumba udongo ambayo ni wewe hapo. Jifunze kumtafuta ndani yako, yupo na hayupo mbali.
Wewe ndiye Taifa takatifu la Mungu na maskani halisi ya Mungu. Wewe ndiye Mungu aliyevaa mwili unaokufa, mwili unaochakaa, na mwenye kusambaratika. Wewe ni taifa la Mungu, ndani yako ni makao halisi ya Mungu. Ukitambua hilo utaanza kuwa huru na mafundisho ya yuko kule Arusha, Abuja, Mwanza, Mwenge au popote, wewe ndiye maskani yake mtazame kisha anza kufurahi pamoja naye. Anakupenda. Acha kutafuta fedha nyingi kumwendea Jerusalem au Oman au popote, huko hayuko bali huyo unayemsafirisha na anayeusafirisha mwili wako mpaka huko ndiye. Yupo ndani yako. Wewe ni Taifa takatifu, tambua hivyo na shangilia wewe si mnyonge hivyo usiruhusu unyonge tena.
Kabla hujawa kama ulivyo tunaambiwa alikuwepo Mungu tu au kwa jina unaloweza kumwita kwa mazoea yako. Mungu ndiye Baba wa wote, aliye juu ya yote, aliye katika yote, na ndani ya yote. Bila yeye hakuna kinachokuwa kama kilivyo. Imeandikwa alifinyanga udongo na kupuliza ndani yake roho wa uhai, kisha binadamu akawa nafsi hai. Mungu aliye roho anaingia katika nyumba aliyoifinyanga mwenyewe. Tukiondoa roho wa Mungu aletaye uhai ndani yako wewe ni nchi, wewe ni udongo. Kwa Mungu aliye mtakatifu sana kuamua kuacha utukufu wake na kujihengea nyumba ya udongo na kisha kukaa huko, wewe umefanyika nchi Takatifu ( Holly Land), give thanks to God. Mpe utukufu Mungu wewe ni wa kipekee you are gods na kati yenu hakuna aliye zaidi ya mwingine.
Acha kuheshimu au kuhangaika kutafuta nchi takatifu, wewe ndiye nchi takatifu. Acha kutafuta mahala patakatifu pa kuhiji wewe ndiye mahala penyewe alipopachagua Mungu.. hiji ndani yako na endelea kumtolea Mungu Dhabihu za shukrani. Utu wako ndiyo maskani yake Mungu ambayo yanapendeza kama nini? Je unayatamani makao ya Bwana? Ingia rohoni mwako kutana Naye maana imeandikwa je hamjui kwamba ninyi ni hekalu la roho mtakatifu. Mungu ni roho na ajili yake wewe upo na kwa njia yake ukafanyika kuwa kama ulivyo. Wewe ni maskani matakatifu ya Mungu mwenyewe. Acha kukimbiakimbia kumtafuta kule na kule, yeye yupo ndani ya nyumba udongo ambayo ni wewe hapo. Jifunze kumtafuta ndani yako, yupo na hayupo mbali.
Wewe ndiye Taifa takatifu la Mungu na maskani halisi ya Mungu. Wewe ndiye Mungu aliyevaa mwili unaokufa, mwili unaochakaa, na mwenye kusambaratika. Wewe ni taifa la Mungu, ndani yako ni makao halisi ya Mungu. Ukitambua hilo utaanza kuwa huru na mafundisho ya yuko kule Arusha, Abuja, Mwanza, Mwenge au popote, wewe ndiye maskani yake mtazame kisha anza kufurahi pamoja naye. Anakupenda. Acha kutafuta fedha nyingi kumwendea Jerusalem au Oman au popote, huko hayuko bali huyo unayemsafirisha na anayeusafirisha mwili wako mpaka huko ndiye. Yupo ndani yako. Wewe ni Taifa takatifu, tambua hivyo na shangilia wewe si mnyonge hivyo usiruhusu unyonge tena.
NCHI TAKATIFU (HOLLY LAND)
Nchi Takatifu ( Holly Land)
Kabla hujawa kama ulivyo tunaambiwa alikuwepo Mungu tu au kwa jina unaloweza kumwita kwa mazoea yako. Mungu ndiye Baba wa wote, aliye juu ya yote, aliye katika yote, na ndani ya yote. Bila yeye hakuna kinachokuwa kama kilivyo. Imeandikwa alifinyanga udongo na kupuliza ndani yake roho wa uhai, kisha binadamu akawa nafsi hai. Mungu aliye roho anaingia katika nyumba aliyoifinyanga mwenyewe. Tukiondoa roho wa Mungu aletaye uhai ndani yako wewe ni nchi, wewe ni udongo. Kwa Mungu aliye mtakatifu sana kuamua kuacha utukufu wake na kujihengea nyumba ya udongo na kisha kukaa huko, wewe umefanyika nchi Takatifu ( Holly Land), give thanks to God. Mpe utukufu Mungu wewe ni wa kipekee you are gods na kati yenu hakuna aliye zaidi ya mwingine.
Acha kuheshimu au kuhangaika kutafuta nchi takatifu, wewe ndiye nchi takatifu. Acha kutafuta mahala patakatifu pa kuhiji wewe ndiye mahala penyewe alipopachagua Mungu.. hiji ndani yako na endelea kumtolea Mungu Dhabihu za shukrani. Utu wako ndiyo maskani yake Mungu ambayo yanapendeza kama nini? Je unayatamani makao ya Bwana? Ingia rohoni mwako kutana Naye maana imeandikwa je hamjui kwamba ninyi ni hekalu la roho mtakatifu. Mungu ni roho na ajili yake wewe upo na kwa njia yake ukafanyika kuwa kama ulivyo. Wewe ni maskani matakatifu ya Mungu mwenyewe. Acha kukimbiakimbia kumtafuta kule na kule, yeye yupo ndani ya nyumba udongo ambayo ni wewe hapo. Jifunze kumtafuta ndani yako, yupo na hayupo mbali.
Wewe ndiye Taifa takatifu la Mungu na maskani halisi ya Mungu. Wewe ndiye Mungu aliyevaa mwili unaokufa, mwili unaochakaa, na mwenye kusambaratika. Wewe ni taifa la Mungu, ndani yako ni makao halisi ya Mungu. Ukitambua hilo utaanza kuwa huru na mafundisho ya yuko kule Arusha, Abuja, Mwanza, Mwenge au popote, wewe ndiye maskani yake mtazame kisha anza kufurahi pamoja naye. Anakupenda. Acha kutafuta fedha nyingi kumwendea Jerusalem au Oman au popote, huko hayuko bali huyo unayemsafirisha na anayeusafirisha mwili wako mpaka huko ndiye. Yupo ndani yako. Wewe ni Taifa takatifu, tambua hivyo na shangilia wewe si mnyonge hivyo usiruhusu unyonge tena.
Kabla hujawa kama ulivyo tunaambiwa alikuwepo Mungu tu au kwa jina unaloweza kumwita kwa mazoea yako. Mungu ndiye Baba wa wote, aliye juu ya yote, aliye katika yote, na ndani ya yote. Bila yeye hakuna kinachokuwa kama kilivyo. Imeandikwa alifinyanga udongo na kupuliza ndani yake roho wa uhai, kisha binadamu akawa nafsi hai. Mungu aliye roho anaingia katika nyumba aliyoifinyanga mwenyewe. Tukiondoa roho wa Mungu aletaye uhai ndani yako wewe ni nchi, wewe ni udongo. Kwa Mungu aliye mtakatifu sana kuamua kuacha utukufu wake na kujihengea nyumba ya udongo na kisha kukaa huko, wewe umefanyika nchi Takatifu ( Holly Land), give thanks to God. Mpe utukufu Mungu wewe ni wa kipekee you are gods na kati yenu hakuna aliye zaidi ya mwingine.
Acha kuheshimu au kuhangaika kutafuta nchi takatifu, wewe ndiye nchi takatifu. Acha kutafuta mahala patakatifu pa kuhiji wewe ndiye mahala penyewe alipopachagua Mungu.. hiji ndani yako na endelea kumtolea Mungu Dhabihu za shukrani. Utu wako ndiyo maskani yake Mungu ambayo yanapendeza kama nini? Je unayatamani makao ya Bwana? Ingia rohoni mwako kutana Naye maana imeandikwa je hamjui kwamba ninyi ni hekalu la roho mtakatifu. Mungu ni roho na ajili yake wewe upo na kwa njia yake ukafanyika kuwa kama ulivyo. Wewe ni maskani matakatifu ya Mungu mwenyewe. Acha kukimbiakimbia kumtafuta kule na kule, yeye yupo ndani ya nyumba udongo ambayo ni wewe hapo. Jifunze kumtafuta ndani yako, yupo na hayupo mbali.
Wewe ndiye Taifa takatifu la Mungu na maskani halisi ya Mungu. Wewe ndiye Mungu aliyevaa mwili unaokufa, mwili unaochakaa, na mwenye kusambaratika. Wewe ni taifa la Mungu, ndani yako ni makao halisi ya Mungu. Ukitambua hilo utaanza kuwa huru na mafundisho ya yuko kule Arusha, Abuja, Mwanza, Mwenge au popote, wewe ndiye maskani yake mtazame kisha anza kufurahi pamoja naye. Anakupenda. Acha kutafuta fedha nyingi kumwendea Jerusalem au Oman au popote, huko hayuko bali huyo unayemsafirisha na anayeusafirisha mwili wako mpaka huko ndiye. Yupo ndani yako. Wewe ni Taifa takatifu, tambua hivyo na shangilia wewe si mnyonge hivyo usiruhusu unyonge tena.
Kimbunga Kenneth( Rainstorms)
JINSI YA KUJIOKOA NA KIMBUNGA (RAINSTORMS)
Kama tulivyokwisha sikia kwenye chombo chetu cha Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania kuna maeneo ambayo yatakumbwa na kimbunga kilichopewa jina Keneth mapema kuanzia siku ya kesho japo hatujajuwa muda rasmi lakini kinaweza kikawasili hata kuanzia leo usiku.
Tumeona ni jambo jema ku share nanyi jambo hili ili kuokoa maisha na kupunguza madhara yatakayo jitokeza kule kwa wenzetu kusini mwa Tanzania.
Kiukweli kwa mazingira na hali ya kimaisha kwa sisi waTanzania sio rahisi kujikoa na majanga haya ya vimbunga kutokana na aina ya nyumba zetu pamoja na kukosa mazingira au maeneo ya Emergency kwa matukio kama haya au kuhama kwa muda.
JINSI YA KUJIOKOA
Zaidi ya kuhama eneo la tukio Huwezi kuzuia kimbunga hata siku moja na madhara yake huwa ni makubwa sana lakini vipo vitu vichache sana ambavyo ukivifuata vinaweza kukupunguzia madhara ki mwili.
Kimbunga kitawasili na Mvua kali sana yenye upepo mkali kwahivyo baada ya kuona hivyo fuata mambo haya yafuatayo.
1. Kitu cha kwanza usi panic tuliza moyo wako na usiwe na Papara na pia punguza woga.
2. Funga milango yote ya nyumba yako pamoja na madirisha yote usiache wazi hata sehemu moja.
3. Usikae karibu na Madirisha au Milango kwasababu maeneo hayo hayatakuwa si salama kipindi upepo huo mkali unapita.
4. Tunashauri wazazi mkae karibu na watoto wenu kipindi chote ambacho upepo utakuwa unapita.
5. Kama unaishi kwenye nyumba ambayo unahisi haitaweza kuhimili upepo mkali kwa siku ya leo omba hifadhi kwenye nyumba ambayo kuna uwezekano ikahimili upepo mkali.
6. Kuna uwezekano upepo ukaona umeizidi nyumba yako na sasa unataka kuangusha nyumba. Usitoke na kukimbia hovyo. Wewe na watu wako ingieni chini ya kitu kigumu kama vile meza kwasababu utakapo toka nje huku upepo mkali ukiwa unavuma madhara yake huenda yakawa makubwa kwasababu upepo utapeperusha Mabati, miti na vitu vingine ambavyo vikikukuta vinawedha kuleta madhara makubwa.
7. Kuna uwezekano kimbunga kikaleta maji mengi sana na kuanza kujaa ndani. Ikitokea hali hii basi mtalazimika kutoka ndani kwa usalama. Shikaneni mikono na hakikisheni mnatembea pembezo pembezo msitembee maeneo ya wazi kutokana na vitu vitavyokuwa vinapeperushwa vikiwakuta itakuwa ni madhara makubwa. Tembeeni kwa usalama na kwa haraka muwahi sehemu ambayo mtaona itakuwa na usalama.
8. Kama kimbunga kitajaza maji mengi basi ni vema yakaandaliwa madumu matupu kisha yafungwe vizuri yasipitishe hewa yatasaidia kuelea kwa wale ambao watakuwa hawajiwezi kwa kuogelea haswa watoto na wazee.
Mambo hayo kadhaa nimejaribu kupitia katika website mbalimbali kusoma kisha kuwaleteeni hapa.
Kusoma kwa undani zaidi kuhusu kumbunga hiki bonyeza Link hiyo hapo chini.
https://bbc.in/2ZvoKEn
OMBI
Tunaomba ku share post hii mara nyingi uwezavyo iwafikie wale wote watakaoweza kuiona kwasababu madhara ya kimbunga IDAI kilicho tokea nchi za jirani kusini mwa Tanzania wiki kadhaa zilizopita yalikuwa ni makubwa saana na tuliondokewa na ndugu zetu 960 na zaidi Hakuna mtu aliejuwa kuwa madhara yatakuwa makubwa kiasi kile na mpaka sasa Takribani watu Milioni 3 bado wanahitaji misaada ya kibiinaadamu
Unakaribishwa kuchangia chochote kile kwenye comment kwaajili ya ushauri kwa wenzetu ambao watakumbwa na Janga hilo.
Kama tulivyokwisha sikia kwenye chombo chetu cha Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania kuna maeneo ambayo yatakumbwa na kimbunga kilichopewa jina Keneth mapema kuanzia siku ya kesho japo hatujajuwa muda rasmi lakini kinaweza kikawasili hata kuanzia leo usiku.
Tumeona ni jambo jema ku share nanyi jambo hili ili kuokoa maisha na kupunguza madhara yatakayo jitokeza kule kwa wenzetu kusini mwa Tanzania.
Kiukweli kwa mazingira na hali ya kimaisha kwa sisi waTanzania sio rahisi kujikoa na majanga haya ya vimbunga kutokana na aina ya nyumba zetu pamoja na kukosa mazingira au maeneo ya Emergency kwa matukio kama haya au kuhama kwa muda.
JINSI YA KUJIOKOA
Zaidi ya kuhama eneo la tukio Huwezi kuzuia kimbunga hata siku moja na madhara yake huwa ni makubwa sana lakini vipo vitu vichache sana ambavyo ukivifuata vinaweza kukupunguzia madhara ki mwili.
Kimbunga kitawasili na Mvua kali sana yenye upepo mkali kwahivyo baada ya kuona hivyo fuata mambo haya yafuatayo.
1. Kitu cha kwanza usi panic tuliza moyo wako na usiwe na Papara na pia punguza woga.
2. Funga milango yote ya nyumba yako pamoja na madirisha yote usiache wazi hata sehemu moja.
3. Usikae karibu na Madirisha au Milango kwasababu maeneo hayo hayatakuwa si salama kipindi upepo huo mkali unapita.
4. Tunashauri wazazi mkae karibu na watoto wenu kipindi chote ambacho upepo utakuwa unapita.
5. Kama unaishi kwenye nyumba ambayo unahisi haitaweza kuhimili upepo mkali kwa siku ya leo omba hifadhi kwenye nyumba ambayo kuna uwezekano ikahimili upepo mkali.
6. Kuna uwezekano upepo ukaona umeizidi nyumba yako na sasa unataka kuangusha nyumba. Usitoke na kukimbia hovyo. Wewe na watu wako ingieni chini ya kitu kigumu kama vile meza kwasababu utakapo toka nje huku upepo mkali ukiwa unavuma madhara yake huenda yakawa makubwa kwasababu upepo utapeperusha Mabati, miti na vitu vingine ambavyo vikikukuta vinawedha kuleta madhara makubwa.
7. Kuna uwezekano kimbunga kikaleta maji mengi sana na kuanza kujaa ndani. Ikitokea hali hii basi mtalazimika kutoka ndani kwa usalama. Shikaneni mikono na hakikisheni mnatembea pembezo pembezo msitembee maeneo ya wazi kutokana na vitu vitavyokuwa vinapeperushwa vikiwakuta itakuwa ni madhara makubwa. Tembeeni kwa usalama na kwa haraka muwahi sehemu ambayo mtaona itakuwa na usalama.
8. Kama kimbunga kitajaza maji mengi basi ni vema yakaandaliwa madumu matupu kisha yafungwe vizuri yasipitishe hewa yatasaidia kuelea kwa wale ambao watakuwa hawajiwezi kwa kuogelea haswa watoto na wazee.
Mambo hayo kadhaa nimejaribu kupitia katika website mbalimbali kusoma kisha kuwaleteeni hapa.
Kusoma kwa undani zaidi kuhusu kumbunga hiki bonyeza Link hiyo hapo chini.
https://bbc.in/2ZvoKEn
OMBI
Tunaomba ku share post hii mara nyingi uwezavyo iwafikie wale wote watakaoweza kuiona kwasababu madhara ya kimbunga IDAI kilicho tokea nchi za jirani kusini mwa Tanzania wiki kadhaa zilizopita yalikuwa ni makubwa saana na tuliondokewa na ndugu zetu 960 na zaidi Hakuna mtu aliejuwa kuwa madhara yatakuwa makubwa kiasi kile na mpaka sasa Takribani watu Milioni 3 bado wanahitaji misaada ya kibiinaadamu
Unakaribishwa kuchangia chochote kile kwenye comment kwaajili ya ushauri kwa wenzetu ambao watakumbwa na Janga hilo.
Monday, January 28, 2019
TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA POLISI.
_*KUTOKA JESHI LA POLICE:*_
_*USALAMA WA MAISHA YAKO*_
☆ _*Usinunue simu za Android kwa mtu usiyemjua*. Hiyo ni hatari kwani hujui huyo jamaa kaitoa wapi, mwisho wa siku unapewa kesi ya wizi au mauaji._ _Inawezekana simu hiyo iliibiwa kwa mtu aliyeuawa._
☆ _*Usimpe mtu usiyemjua* simu yako apige sehemu yoyote._
_*Unapoiona line njiani ipo chini*, usitake kuiokota na kuiweka simuni mwako ujue ina shilingi ngapi ili uchukue salio._
☆ _*Simu inapoibiwa* au_
_mwenye simu kuuawa, line hutupwa, unapoiweka simuni mwako,simuyako inahusishwa na tukio hilo_
☆ _*Unapoweka salio,* hakikisha karatasi ya vocha unaichana. Unapoitupa, watu wanaweza kufanya mauaji, wakachukua karatasi ya vocha ile na kuweka sehemu ya tukio au pale ulipoitupa kukatokea tukio na wewe kuhusishwa._
☆ _*Usikubali kumsajilia mtu line* yake kwa jina lako, hata kama baba yako, usikubali._
☆ _*Kumbuka namba yako umesajiliwa*, moja ya matukio hayo yakitokea na namba yako kuonekana, moja kwa moja unakuwa mtuhu-miwa namba moja._
☆ _*Wengi wamepewa kesi za mauaji*, wizi bila kujua. Polisi wapo kazini, wanapoona vidhibiti wanakuchukua kwani hawatojua kama umehusika au la. Kuweni makini ili usije kuingia matatizoni, simu yako, fedha zako, ukifanya kisicho sahihi kama uzembe, utaishia pabaya._
Kutoka Cyber Crimes
_*SIMU YAKO JEMBE LAKO*_ 🙏🏼
_*SHARE UJUMBE HUU UMPE ONYO NA MWENZAKO.*_
_*USALAMA WA MAISHA YAKO*_
☆ _*Usinunue simu za Android kwa mtu usiyemjua*. Hiyo ni hatari kwani hujui huyo jamaa kaitoa wapi, mwisho wa siku unapewa kesi ya wizi au mauaji._ _Inawezekana simu hiyo iliibiwa kwa mtu aliyeuawa._
☆ _*Usimpe mtu usiyemjua* simu yako apige sehemu yoyote._
_*Unapoiona line njiani ipo chini*, usitake kuiokota na kuiweka simuni mwako ujue ina shilingi ngapi ili uchukue salio._
☆ _*Simu inapoibiwa* au_
_mwenye simu kuuawa, line hutupwa, unapoiweka simuni mwako,simuyako inahusishwa na tukio hilo_
☆ _*Unapoweka salio,* hakikisha karatasi ya vocha unaichana. Unapoitupa, watu wanaweza kufanya mauaji, wakachukua karatasi ya vocha ile na kuweka sehemu ya tukio au pale ulipoitupa kukatokea tukio na wewe kuhusishwa._
☆ _*Usikubali kumsajilia mtu line* yake kwa jina lako, hata kama baba yako, usikubali._
☆ _*Kumbuka namba yako umesajiliwa*, moja ya matukio hayo yakitokea na namba yako kuonekana, moja kwa moja unakuwa mtuhu-miwa namba moja._
☆ _*Wengi wamepewa kesi za mauaji*, wizi bila kujua. Polisi wapo kazini, wanapoona vidhibiti wanakuchukua kwani hawatojua kama umehusika au la. Kuweni makini ili usije kuingia matatizoni, simu yako, fedha zako, ukifanya kisicho sahihi kama uzembe, utaishia pabaya._
Kutoka Cyber Crimes
_*SIMU YAKO JEMBE LAKO*_ 🙏🏼
_*SHARE UJUMBE HUU UMPE ONYO NA MWENZAKO.*_
Subscribe to:
Posts (Atom)