Search This Blog

Monday, January 7, 2013

  • ULINZI WA HAKI ZA BINADAMU KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO

    1. Katiba itatambua na kulinda haki na uhuru muhimu wa binadamu zinazotambulika Kama haki za binadamu za kizazi cha kwanza, yaani haki zote zilizoainishwa katika Sehemu ya Tatu ya Sura ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, na zile zilizoainishwa katika mikataba mbali mbali ya kimataifa ya haki za binadamu.

    2. Katiba itatambua na kulinda haki zote za binadamu zinazotambulika Kama haki za kizazi cha pili za binadamu kama zilivyoainishwa katika ibara ya 11 ya Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano, na zilizoainishwa katika mikataba mbali mbali ya kimataifa inayohusu haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Haki hizo ni pamoja na:
    ...
    (a) Haki ya Mtu kufanya kazi;

    (b) Haki ya kupata elimu;

    (c) Haki ya kupata msaada kutoka kwa jamii wakati wa uzee, maradhi au hali ya ulemavu na katika hali nyinginezo za mtu kuwa hajiwezi.

    3. Katiba itatambua kwamba Wananchi ndio wamiliki wa rasilimali asilia za maeneo wanakoishi Kama vile ardhi, madini, mafuta, gesi asilia, misitu/wanyama pori na rasilimali uvuvi na kwamba jukumu la Serikali ni kuwezesha Wananchi wa maeneo husika kunufaika na umilikaji huo wa rasilimali asilia.

    4. Wananchi hawatanyang'anywa rasilimali zao asilia na mamlaka za Serikali matumizi na watu au taasisi nyingine ya rasilimali asilia za Wananchi bila kwanza Wananchi watakaoathiriwa na unyang'anyi au matumizi hayo kutoa ridhaa yao baada ya kupatiwa taarifa zote na kamili zinazohusu matumizi yanayotarajiwa ya rasilimali hizo na athari za matumizi hayo kwa mazingira, kiuchumi na kijamii (the right of prior informed consent).

    5. Wananchi, Kama wamiliki wa msingi wa rasilimali asilia, watakuwa na haki ya kulipwa mrahaba kwa ajili ya matumizi ya watu au taasisi nyingine ya rasilimali asilia za Wananchi, wakati mamlaka za Serikali za mitaa, Majimbo na Serikali Kuu zitakuwa na haki ya kutoza kodi mapato yatakayotokana na matumizi ya rasilimali hizo.

    6. Haki za binadamu zilizotambuliwa na Katiba hazitawekewa vizingiti au kuminywa kwa kutumia sheria za kawaida za Bunge au vizingiti vilivyowekwa na Katiba yenyewe (clawback/derogation clauses) ambavyo havilingani na misingi inayokubalika ya kimataifa inayohusu haki za binadamu.


No comments:

Post a Comment